Pages

vendredi 6 février 2015

MAREKANI YATAKA BARAZA LA USALAMA LA UMOJA WA MATAIFA KUIWEKEA SUDANI VIKWAZO VYA SILAHA


Licha ya makubaliano ya hivi karibuni kati ya viongozi wawili mahasimu wa Sudan Kusini, Serikali ya Marekani kupitia waziri wake wa mambo ya kigeni John Kerry, ametaka baraza la usalama la umoja wa mataifa kupitisha azimio la kuiwekea vikwazo vya kununua na kuuziwa silaha kwa nchi ya Sudan Kusini.

Licha ya mijadala inayofanyika mara kwa mara kwenye baraza la usalama la Umoja wa mataifa kutaka nchi hiyo kuwekewa vikwazo, kumekuwa na kusuasua kufikiwa kwa maazimio ya pamoja kuhusu hatua za kuchukua dhidi ya rais Salva Kiir na mwenzake Dr Riek Machar.

Hivi sasa Serikali ya Marekani inataka kupitishwa kwa azimio maalumu kuhusu nchi ya Sudan Kusini na kwamba viongozi wake ni lazima wawekewe vikwazo kushinikiza kufikiwa kwa suluhu nchini humo.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire

KINACHOFANYWA NA RAIS NKURUNZIZA KWA SASA NDIO ULE MCHEZO WA NDANI?

Mkanganyiko umeendelea kushuhudiwa katika chama tawala nchini Burundi cha CNDD-FDD, chama ambacho hapo awali kilileta matumaini ya kuwau...