Pages

mercredi 18 février 2015

JESHI LA NIGERIA LAJIGAMBA KUWAUA BOKO HARAM WAKATI KUNDI HILO LIKITISHIA KUZUIA UCHAGUZI




Jeshi la Nigeria linasema limewaua wanamgambo zaidi ya 300 wa Boko Haram katika mji wa Monguno katika jimbo la Borno Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo.
Msemaji wa jeshi Chris Olukolade amesema licha ya kuwaua wanagambo hao imefanikiwa pia kuwakamata baadhi yao.

Wakati jeshi likisema hayo, kiongozi wa kundi la Boko Haram Abubakar Shekau kupitia ujumbe wake mpya uliotolewa katika mkanda wa Video amesema atahakikisha kuwa kundi lake linasambaratisha uchaguzi wa urais uliopangwa kufanyika tarehe 28 mwezi ujao.

Tume ya Uchaguzi nchini humo iliahirisha Uchaguzi huo baada ya jeshi kusema kuwa halikuwa na uwezo wa kutoa ulinzi kwa wananchi wakati huo na kuomba wiki sita kukabiliana na kundi hilo.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire

KINACHOFANYWA NA RAIS NKURUNZIZA KWA SASA NDIO ULE MCHEZO WA NDANI?

Mkanganyiko umeendelea kushuhudiwa katika chama tawala nchini Burundi cha CNDD-FDD, chama ambacho hapo awali kilileta matumaini ya kuwau...