Pages

vendredi 11 avril 2014

JESHI LA KENYA LAFAANIKIWA KUWAOKOA RAIA WAKE WAWILI KUTOKA MIKONONI MWA AL SHABAB

Jeshi la ulinzi nchini Kenya hii leo limetangaza kufanikiwa kuwaokoa raia wake wawili waliokuwa wanashikiliwa mateka toka mwaka 2011 na wanamgambo wa kundi la Al-Shabab nchini Somalia.

Msemaji wa jeshi la ulinzi nchini humo, Kanali Willy Wesonga amethibitisha jeshi la nchi yake kuwaokoa raia hao wawili waliotambuliwa kwa majina ya James Kairie Gichuhi aliyekuwa dereva wa shirika la Care International na Daniel Njuguna Wanyoike anayeelezwa kuwa mfanyakazi wa shirika moja la usafirishaji dawa nchini humo.


Raia hao waliokolewa na wanajeshi wa Kenya walioko nchini Somalia chini ya mwavuli wa vikosi vya Umoja wa Afrika AMISOM ambapo walikuwa wanashikiliwa mateka na wanamgambo hao kaskazini mwa nchi ya kenya kwenye mpaka na nchi ya Somalia toka mwaka 2011.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire

KINACHOFANYWA NA RAIS NKURUNZIZA KWA SASA NDIO ULE MCHEZO WA NDANI?

Mkanganyiko umeendelea kushuhudiwa katika chama tawala nchini Burundi cha CNDD-FDD, chama ambacho hapo awali kilileta matumaini ya kuwau...