Pages

mardi 22 avril 2014

KUNDI LA AL SHABAB LATEKELEZA MAUAJI YA WABUNGE WAWILI KWA MUDA WA SIKU MBILI


Mbunge mmoja nchini Somalia amepigwa risase na kupoteza maisha papo hapo jijini Mogadishu, ikiwa ni siku moja baada ya kuripotiwa mauaji ya mbunge mwingine wa serikali katika mlipuko wa bomu iliotegwa katika gari lake, mauaji ambayo yametekelezwa na wanamgambo wa Al Shabab.


Abdiaziz Isak Mursal ameuawa jumanne karibu na nyumbani kwake katika kata ya Madina kusini mwa mji mkuu na watu wawili waliokuwa na silaha waliotimka baada ya kutekeleza mauaji hayo.
Duru za polisi zimethibitisha kuuawa kwa mbunge huyo aliepigwa risase na kupoteza maisha papo hapo.
Kundi la Al Shabab limejigamba kutekeleza shambulio hilo, na lile lilitokea jana siku ya Jumatatu dhidi ya mbunge Isak Mohamed Ali aliepoteza maisha huku mwingine Mohamed Abdi akujeruhiwa.
Msemaji wa kundi la Al Shabab Abdulaziz Abu Musab amesema wao ndio wanaohusika na matukio hayo dhidi ya wabunge wanaoendesha kazi kwa faida za wageni na kuwatumia ujumbe mzito wabunge wengine wa serikali ya Somalia.
Al Shabab wameahidi kumuawa mbunge mmoja baada ya mwingine.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire

KINACHOFANYWA NA RAIS NKURUNZIZA KWA SASA NDIO ULE MCHEZO WA NDANI?

Mkanganyiko umeendelea kushuhudiwa katika chama tawala nchini Burundi cha CNDD-FDD, chama ambacho hapo awali kilileta matumaini ya kuwau...