Pages

mercredi 12 mars 2014

KESI YA WATUHUMIWA WA JARIBIO LA MAPINDUZI NCHINI SUDANI KUSINI YAANZA KUSIKILIZWA JIJINI JUBA


Kesi ya maafisa wakuu wanne wa chama cha SPLM wanaotuhumiwa ugaidi, uasi na jaribio la kuipindua serikali ya Rais Salva Kiir imeanza kusikilizwa jana mjini Juba nchini Sudani Kusini.

Watuhumiwa hao ni Pagan Amum, katibu mkuu wa zamani wa SPLM, Waziri wa zamani wa Usalama Oyai Deng Ajak, Ezekiel Lol Gatkuoth aliyekuwa Balozi wa Sudan Kusini nchini Marekani na Naibu waziri wa ulinzi Makaj D' Agoot ambao ni washirika wa karibu wa Riek Machar , aliyekuwa makamu wa rais.

Mawakili wa watuhumiwa hao wanazungumzia kesi hiyo kuwa ya kisiasa na njama za kuwadhoofisha wanasiasa hao nchini humo.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire

KINACHOFANYWA NA RAIS NKURUNZIZA KWA SASA NDIO ULE MCHEZO WA NDANI?

Mkanganyiko umeendelea kushuhudiwa katika chama tawala nchini Burundi cha CNDD-FDD, chama ambacho hapo awali kilileta matumaini ya kuwau...