
Balozi
maalumu wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na masuala ya
kupambana na maambukizi ya UKIMWI barani Afrika, Speciosa
Wandira-Kazimbwe ambaye pia aliwahi kuwa makamu wa rais wa Uganda,
amesema sheria hiyo inaongeza uwepo wa vitendo vya ubaguzi dhidi ya
jamii ya watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja.
Kazimbwe
amesema hatua hiyo inarudisha nyuma juhudi za Uganda kupambana na
maambukizi mapya, ambapo mwaka 2012 kulikuwa na wagonjwa milioni 1.5
pekee lakini kumekuwa na ongezeko la wagonjwa wapya laki 1 na elfu
40.
Aucun commentaire:
Enregistrer un commentaire