Pages

vendredi 14 mars 2014

KATIBU MKUU WA UMOJA WA MATAIFA BAN KI MOON AIONYA SERIKALI YA BURUNDI KUHUSU HALI INAYOJIRI NCHINI HUMO

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon ameionya serikali ya Burundi kuhusu kuendelea kuminywa kwa uhuru wa kujieleza na haki ya kufanya mikusanyiko ambapo ametoa wito kwa serikali na vyama vya siasa kujiepusha na haraKati zozote ambazo zinaweza kuchangia kutokea machafuko.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na msemaji wa katibu mkuu Ban, imesema kuwa kiongozi huyo ameguswa na hali tete ya kisiasa inayoendelea kushuhudiwa nchini humo kati ya wanaharakati wa upinzani na polisi.

Katibu mkuu Ban amelaani hatua ya Serikali kukataza mikusanyiko ya kisiasa ya vyama vya upinzani na hatua ya polisi kutumia nguvu dhidi ya wapinzani huku kundi la vijana wa chama tawala wakipewa nafasi ya kufanya mikusanyiko.

Kiongozi huyo amesema ili nchi ya Burundi ifanye uchaguzi ulio huru na haki ifikapo mwaka 2015 ni lazima serikali iruhusu uhuru wa demokrasia kwa kutoa fursa sawa kwa upinzani.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire

KINACHOFANYWA NA RAIS NKURUNZIZA KWA SASA NDIO ULE MCHEZO WA NDANI?

Mkanganyiko umeendelea kushuhudiwa katika chama tawala nchini Burundi cha CNDD-FDD, chama ambacho hapo awali kilileta matumaini ya kuwau...