Pages

mardi 10 mars 2015

SIMONE GBAGBO AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA 20 JELA

Simone Gbagbo mke wa rais wa zamani wa cote di'Ivoire Larent Gbagbo amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kutokana na makosa yaliotendeka baada ya uchaguzi wa mwaka 2010-2011.


Jopo la majaji wote kwa pamoja wamemuhukumu Simone Gbagbo kifungo cha miaka 20 kutokana na ushiriki wake katika harakati za vurugu na kuyumbisha usalama wa taifa.


Taarifa hii imetolewa na jaji mkuu Tahirou Dembele baada ya jopo hilo la majaji kukutana kwa muda wa saa tisa. Kesi hiyo ilianza kusikilizwa tangu desemba mwaka jana.

SERIKALI YA BURUNDI YAPUUZIA WITO WA HUSSEIN RADJABU KINARA ZAMANI WA CHAMA TAWALA CHA CNDD-FDD

Hussein Radjabu mwenyekiti zamani wa chama tawala cha CNDD-FDD















Baada ya mwenyekiti zamani wa chama tawala nchini Burundi Hussein Radjabu kujitokeza kwenye vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa ikiwa ni majuma kadhaa baada ya kuwepo kwa taarifa za kutoroka jela na kutowa wito kwa Jumuiya ya kimataifa kutovumilia uvunjifu wa sheria ya Burundi kwa kumruhusu Nkurunziza kuwania uchaguzi kwa muhula wa 3, serikali imesema Hussein Radjabu ni mtu anaependa uasi, hivyo hana nafasi kwa sasa nchini Burundi.

Hussein Radjabu Mwenyekiti zamani wa chama tawala nchini Burundi cha CNDD-FDD amezungumza kwa mara ya kwanza tangu kuwepo na taarifa za kutoroka kwake katika jela kuu la Mpimba jijini Bujumbura.

Akihojiwa na idhaa mbalimbali za kimataifa, Hussein Radjabu amesema Kwa sasa yupo katika eneo salama, pamoja na wananchi.

Katika mahojiano hayo, Hussein Rajabu amesema hakutoroka jela kama inavyoelzwa huku na kule bali kilichotokea faili lake lilikuwa tayari, lakini rais Nkurunziza alikuwa bado amebana kwa sababu azijuazo mwenyewe, lakini kutokana na watu wa karibu waliokuwa pamoja katika harakati za kuwania demokrasia, hawakupenda kuona naendelea kueshi katika jela katika kipindi hiki ambacho kulikuw ana mpango wa kuendesha vurugu katika jela ili wamzuri.

Akieleza namna alivyoondoka katika jela kuu ka mpimba, kinara huyo zamani wa CNDD-FDD amesema aliondoka kwa heshima na tahadhwima hadi eneo alipo kwa wakati huu.

Akizungumzia kuhusu hali ya siasa nchini mwake na iwapo ana nia ya kurejea nyumbani kushiriki kwenye uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika mwezi June mwaka huu, mwenyekiti huyo wa zamani wa CNDD-FDD amesema tatizo lililopo sio ushiriki wake au la bali ni utawala uliopo hautaki kuheshimu misingi ya demokrasia.

Willy Nyamitwe msemaji wa rais Nkurunziza
Aidha, kongozi huyo ametowa wito kwa raia na wanasiasa wa Burundi kushikamana ili kuboresha hali ya kisiasa iliopo nchini Burundi ambapo amesema hakuna kinachoendeka, kila kitu kipo katika hali ya sintofaham, hususan maandalizi ya uchaguzi.
Upande wake serikali ya Burundi imesema Radjabu bado hajamaliza kutumikia kifungo chake na kwa vile ni mtu hatari ambaye anaweza kutishia amani nchini Burundi, serikali inajipanga kukabiliana na hali yoyote hiyo kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika hali tulivu.
Msemaji wa rais Nkurunziza kupitia radio ya dunia RFI mapema leo asubuhi amesema Radjabu ni mtu anaefahamika kuwa na tabia ya kuunda makundi ya uasi, hivyo katika kipindi hiki hana nafasi.



lundi 9 mars 2015

MTOTO MWINGINE ALBINO AKATWA KIGANJA CHA MKONO


wakati kampeni ya kupiga vita mauaji ya watu wenye umelavu ikiendelea nchini Tanzania, polisi nchini humoe imsesma hapo jana kwamba mtoto mmoja mwenye ulemavu wa ngozi amekatwa Kiganja cha mkono wake wa kushoto na kundi la watu wasiojulikana.

Baraka Cosmos mtoto mwenye ulemavu wa ngozi alikuwa amelala na mama yake katika kijiji cha Kipenda kusini magharibi mwa Mkoa wa Rukwa ambapo kundi la majambazi waliingia na kumteka mtoto huoyo kabla ya kumjeruhi mama yake.

Duru za polisi zinaeleza kwamba majambazi hao walimpiga mama wa mtoto huyo Prisca Shabani baada ya kukataa kuwapa mwanae na ambapo walitumia panga kwa kukata kiganja cha mkono wa kushoto wa mtoto huyo ambae baadae alipelekwa Hospitalini na mama yake.

Juma lililopita mahakama kaskazini mashariki mwa Tanzania iliwahukumu kunyongwa watu wanne kwa kuhusika na mauji ya mwanamama mmoja mlemavu wa ngozi.

Tukio hili linatokea wakati huu nchini Tanzania kukwa na kampeni kambambe ya kupiga vita mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozo (Albino)

hii ni ishara kwamba kampeni hiyo imefeli, na watu waache kuuza sura kwenye mitandao ya kijamii kwa kuendesha shughuli zisizokuwa na matunda mazuri.

vendredi 6 mars 2015

UMOJA WA ULAYA WAONYA KUHUSU MUHULA WA 3 WA RAIS NKURUNZIZA

Umoja wa Ulaya kupitia muakilishi wake jijini Bujumbura Patrick Spirlet ameonya kuhusu muhula wa 3 wa rais Nkurunziza katika uchaguzi mkuu wa Rais wa Juni nchini humo kwamba unaweza kuzua machafuko katika nchi hiyo.


Joto la kisiasa kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa rais nchini Burundi limeanza kupanda wakati huu kukiwa na shaka kwamba rais Nkurunziza anampango wa kuwania muhula wa 3, jambo ambalo upinzani unasema ni kinyume na katiba ya Burundi na makubalinao ya amani ya Arusha. 

Hata hivyo chama tawala cha CNDD-FDD kinaona kwamba rais Nkurunziza bado ana nafasi ya kuwania kutokana na muhula wa kwanza kuelezwa kwamba hakuchaguliwa na wananchi bali aliteuliwa kupitia bunge.

Patrick Spirlet amesema kumekuwa na maoni tofauti kuhusu muhula huu wa 3, hivyo wametaka maoni hayo yasikilizwe wakati huu tayari kanisa katoliki na Mashirika ya kiraia yameonyesha kupinga hatuwa hiyo ambayo hata hivyo Nkurunziza hajatangaza bayana kwamba atawania muhula mwingine.

Jumuiya ya kimataifa inatiwa wasiwasi na hali ya kisiasa nchini Burundi kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa rais, lakini hii ni mara ya kwanza kabisa kwa Umoja wa Ulaya kuonyesha msimamo wake kuhusu muhula wa 3 wa rais Nkurunziza.

Patrick Spirlet amesema amani nchini Burundi bado ni legelege hivyo inabidi kuheshimu katiba ya nchi hiyo na kuheshimu pia mkataba wa amani wa Arusha uliofikia kusitishwa kwa vita mwaka 1993-2006

Akijibu hoja hii ya Umoja wa Ulaya waziri wa mambo ya nje wa Burundi Laurent Kavakure amesema mkataba wa Arusha sio bibilia ambayo haiwezi kubadilishwa.

mardi 3 mars 2015

WIZARA YA SHERIA NCHINI BURUNDI YASEMA HUSSEIN RAJABU HAJATEKWA BALI AMETOROKA


Wizara ya sheria nchini Burundi imesema kwamba Hussein Radjabu kinara zamani wa chama tawala cha CNDD-FDD hakutekwa bali ametoroka jela kuu la mpimba na kutokomea katika maeneo yasiojulikana bado.

Kulingana na naibi msemaji wa wizara hiyo Bigirimana Eliason amesema Hussein Radjabu ametoroka katika jela kuu la Mpimba katika Usiku wa Jumapili kuamkia Jumatatu March 2 mwaka 2015 akiwa na wafungwa wengine 4, pamoja na askari polisi watatu

Naibu mseji huyo ameeleza kuwa mbali na Hussein Radjabu mfungwa mwingine Ribakare Baudoin maharufu Ndindi, Ndikuma Remy aliekuwa anahusika na Ulinzi wake na Irankunda Sirique liaekuwa mpishi pamoja na polisi watatu.

Hayo yanajiri wakati huu wakili wa Hussein Radjabu Prosper Niyoyankana akitishia kufunguwa mashtaka kutokana na mteja wake huyo ambae haijulikani alipo. Wakili huyo amesema mteja wake amekuwa akifanyiwa madhila na vitisho vya kuuawa alipokua jela.

vendredi 27 février 2015

OMAR AL BASHIR NIPO TAYARI KUNG'ATUKA NIKIANGUKA KWENYE UCHAGUZI MKUU WA RAIS


Rais wa Sudani Omar Hassan Al Bashir anaewania uchaguzi mkuu wa rais unaotarajiwa kufanyika April mwaka huu nchini humo amefahamisha jana kwamba ataachia ngazi iwapo atashindwa kwenye uchaguzi huo uliosusiwa na vyama vikuu vya upinzani.

Akiwa katika kampeni za uchaguzi zilizoanza juma hili katika mji wa Wad Madani kusini mashariki mwa Karthoum, Bashir amesema yupo tyari kujiuzulu kupitia kura katika uchaguzi wa rasis na wa bunge unaotarajiwa kufanyika April 13.

rais Bashir amesema raia ndio wanaojukumu la kuamuwa nani awaongoze kupitia kura. Bashir mwenye umri wa miaka 71 mgombea uraia kwa tikiti ya chama cha National Congress amewatuhumu viongozi wa upinzani kususia uchaguzi na kwamba hakuna nafasi kwa watu ambao wanataka kuongoza nchi kupitia shinikizo ya mataifa ya magharibi kwa kwenda Addis Abeba au Paris.

Vyama vikuu ya upinzani na waasi vilitiliana saini ya kususia uchaguzi huo jijini Adis Abeba nchini Ethiopia na Paris.

mercredi 25 février 2015

ULISHAWAHI KUISKIA HII HAPA ?


Mfano wa Keki ya Birthday

Wataalamu wa kutengeneza keki wanajiandaa kwa shughuli ya utengenezaji wa Keki ya Birthday ya miaka  450 ya jiji la Rio nchini Brezil, itayokuwa na mita 450, ndani yake itakuwa tani 2.5 ya unga wa ngano, tani 2,1 ya sukari, tani 1, 5 ya margarine, yai mia tatu, lita 1000 ya maziwa na mazaga zaga mengine.

Keki hiyo ya mita 450 itawekwa kwenye barabara ya Carioca mjini kati siku ambayo wananchi watakuwa wanasherehekea miaka 450 ya jiji hilo March Mosi mwaka huu, na ambapo kila aliehudhuria sherehe hizo atatakiwa kuhonja.

Mea wa jiji la Rio tayari ametowa kitita kinachokadiriwa kufikia Euro elf 31 kwa ajili ya manunuzi ya vifaa juu ya kutengeneza keki hiyo kubwa kuwa kutengenezwa duniani

KINACHOFANYWA NA RAIS NKURUNZIZA KWA SASA NDIO ULE MCHEZO WA NDANI?

Mkanganyiko umeendelea kushuhudiwa katika chama tawala nchini Burundi cha CNDD-FDD, chama ambacho hapo awali kilileta matumaini ya kuwau...