Pages

mercredi 2 juillet 2014

ADF-NALU YAWEKEWA VIKWAZO NA UMOJA WA MATAIFA


Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeamuwa kuliwekea vikwazo kundi la waasi wa Uganda la ADF lililopiga kambi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Vikwazo hivyo vitawahusu viongozi wa kundi hilo kuwazuia kusafiri na kuhodhi fedha zao.

Vikwazo hivyo vilipendekezwa na mataifa ya Ufaransa, Marekani na Uingereza. ADF linaongozwa tangu mwaka 2007 na Jamil Mukulu ambaye alikuwa mkristo kabla ya kuslim kuwa muislam pamoja na kiongozi wa kijeshi Hood Lukwago ambao wamewekwa katika orodha ya viongozi wa makundi ya kigaidi na Marekani pamoja na Umoja wa Ulaya.

Kundi la ADF ambalo pia linatambulika kwa jina la ADF-NALU linatuhumiwa kuwasajili watoto wenye umri wa chini ya miaka 18 katika kundi hilo na kutekeleza mauaji lakini pia ubakaji dhidi ya kinamama na watoto na kuwashambulia wanajeshi wa kulinda amani nchini DRCongo Monusco.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire

KINACHOFANYWA NA RAIS NKURUNZIZA KWA SASA NDIO ULE MCHEZO WA NDANI?

Mkanganyiko umeendelea kushuhudiwa katika chama tawala nchini Burundi cha CNDD-FDD, chama ambacho hapo awali kilileta matumaini ya kuwau...