Pages

vendredi 9 mai 2014

SALVA KIIR NA RIEK MACHAR WAKAUTANA JIJINI ADDIS ABABA ETHIOPIA

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir na kiongozi wa waasi ambaye pia alikuwa makamu wa rais Riek Machar wanakutana kwa mara ya kwanza ana kwa ana jijini Addis Ababa Ethiopia, kujaribu kupata mwafaka wa kumaliza machafuko yanayoendelea katika taifa lao kwa miezi mitano sasa.

 Kukutana kwa viongozi hawa chini ya wasuluhishi wa mgogoro huo kutoka Mataifa ya Afrika Mashariki IGAD wakiongozwa na Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn kumewapa wananchi wa Sudan Kusini matumaini ya kurejea kwa usalama katika taifa lao.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire

KINACHOFANYWA NA RAIS NKURUNZIZA KWA SASA NDIO ULE MCHEZO WA NDANI?

Mkanganyiko umeendelea kushuhudiwa katika chama tawala nchini Burundi cha CNDD-FDD, chama ambacho hapo awali kilileta matumaini ya kuwau...