Pages

mercredi 18 février 2015

ANGALIA KWA PICHA WATU WALIVYOFURIKA OFIZI ZA RPA BAADA YA KUPEWA DHAMANA KWA BOB RUGURIKA






Lakini baadae mambo yakabadilika na kuwa hivi:



JESHI LA NIGERIA LAJIGAMBA KUWAUA BOKO HARAM WAKATI KUNDI HILO LIKITISHIA KUZUIA UCHAGUZI




Jeshi la Nigeria linasema limewaua wanamgambo zaidi ya 300 wa Boko Haram katika mji wa Monguno katika jimbo la Borno Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo.
Msemaji wa jeshi Chris Olukolade amesema licha ya kuwaua wanagambo hao imefanikiwa pia kuwakamata baadhi yao.

Wakati jeshi likisema hayo, kiongozi wa kundi la Boko Haram Abubakar Shekau kupitia ujumbe wake mpya uliotolewa katika mkanda wa Video amesema atahakikisha kuwa kundi lake linasambaratisha uchaguzi wa urais uliopangwa kufanyika tarehe 28 mwezi ujao.

Tume ya Uchaguzi nchini humo iliahirisha Uchaguzi huo baada ya jeshi kusema kuwa halikuwa na uwezo wa kutoa ulinzi kwa wananchi wakati huo na kuomba wiki sita kukabiliana na kundi hilo.

mardi 17 février 2015

MONUSCO YARIDHISHWA NA HATUWA YA SERIKALI YA DRCONGO KUONGOZA OPERSHENI YA KUWASAKA FDLR



Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo MONUSCO unapongeza dhamira ya serikali ya DRC kuchukua pekee jukumu la kuwasaka waasi wa kihutu wa rwanda wa FDLR walioko Mashariki mwa nchi hiyo kama alivyoamua rais Joseph Kabila.


Kaimu msemaji wa Ujumbe huo Umoja Charles Bambara amesema kuwa pamoja na kupongeza hatua hiyo, MONUSCO itaendelea kufanya kazi kwa ukaribu na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ili kutimiza agizo waliokabidhiwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
 Kulingana na Msemaji huyo, MONUSCO itaendelea kusaidia jeshi la Congo FARDC katika shughuli nyingine za kijeshi dhidi ya vikundi vingine vyenye kumiliki silaha mashariki mwa DRC ikiwa ni pamoja na Kivu ya Kusini, Kivu kaskazini , Butembo, Katanga na mahali pengine.

Kauli hiyo haitofautiani na ile ya Msemaji wa Serikali ya Congo Waziri Lambert Mende ambaye hapo jana katika mkutano na waandishi wa habari amebainisha kuwa MONUSCO kutimiza wajibu wake bila ya kutegemea Jeshi la DRC dhidi ya makundi yote yenye kumiliki silaha kwa vile ni sehemu ya majukumu ya Ujumbe huo.

Kwa upande wake, MONUSCO pia imeahidi kuendelea kutimiza wajibu wake kama ilivyo azma ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa katika shughuli nyingine za kijeshi kwa kushirikaiana na jeshi la DRC amesema Charles Bambara.


lundi 16 février 2015

JESHI LA SERIKALI NA WAASI WATUHUMIWA KUTUMIA WATOTO WADOGO JESHINI


Mashirika ya kutetea haki za binadamu nchini Sudan Kusini yanazituhumu mbande mbili zinazokinzana nchini humo kusajili watoto wadogo walio na umri wa chini ya miaka kuni na mitatu kushiriki kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe, ripoti ambayo serikali ya Juba imekanusha vikali.

Ripoti ya mashirika hayo, imedai kuwa Serikali inashiriki kikamilifu katika kusajili vijana wadogo kujiunga na jeshi lake kwa hiari ama kwa kuwalazimisha wakati waasi wao pia wanatumia watoto kama wanajeshi katima vita vilivyodumu kwa zaidi ya miezi 14 hivi sasa.

Waziri wa habari wa Sudan Kusini, Michael Makuei ametupilia mbali madai ya ripoti hii akisisitiza kuwa jeshi lake bado lina nguvu ya kutosha kupigana bila kutumia watoto.

SERIKALI YA DRCONGO YAKATAA KUSHIRIKIANA NA MONUSCO KATIKA OPERESHENI DHIDI YA FDLR


Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC imesema kuwa imekataa ombi la tume ya Umoja wa mataifa nchini humo kushirikiana na jeshi lake katika operesheni ya kuwasambaratisha wapiganaji wa kundi la FDLR, na kutoa onyo dhidi ya taasisi za kimataifa kuingilia masuala yake ya ndani.

Juma lililopita, tume ya Umoja wa Mataifa ilitangaza kujiondoa katika operesheni ya pamoja na jeshi la Serikali ya DRC, kushiriki operesheni maalumu ya kuwasaka waasi wa Rwanda wa FDLR kwa kile umoja wa mataifa unataka kwanza majenerali wawili wa juu wa jeshi la DRC wafutwe kazi kwa tuhuma za kuhusika na vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu.

Waziri wa habari na msemaji wa serikali ya DRC, Lambert Mende, amesema serikali yake inakataa rasmi ombi la Umoja wa mataifa na kwamba wanajeshi hao hawatafutwa kazi kwa shinikizo na kuzionya taasisi za Umoja huo kutoingilia masuala yake ya ndani.

SAKATA LA KUWANIA MUHULA WA 3 KWA RAIS NKURUNZIZA LAIBUKA TENA


Chama tawala nchini Burundi kimesisitiza kuwa Rais Pierre Nkrunzinza atawania muhula wa tatu wa urais katika uchaguzi mkuu wa mwezi June mwaka huu, iwapo jina lake litapitishwa na chama kuwania nafasi hiyo.

Msimamo huu wa chama tawala cha CNDD-FDD unatolewa wakati huu ambapo muungano wa mashirika ya kiraia nchini Burundi yakitoa wito kwa rais Nkurunzina kutowania muhula mwingine wa urais kuepusha kile walichokiita machafuko nchini humo.

Msemaji wa Rais, Willy Nyamitwe amesema kuwa rais Nkurunzinza atawania kiti cha urais katika uchaguzi ujao iwapo kamati kuu ya chama itamteua kufanya hivyo kulingana na katiba huku akiwaonya watu wanaotaka kuchochea vurugu nchini humo.


Kiongozi huyo ameongeza kuwa vyombo vya usalama pamoja na vyombo vya sheria vitawachukulia hatua wale wote ambao watabainika kupanga njama za kuchochea machafuko nchini humo kabla na hata wakati wa uchaguzi mkuu.

Mashirika ya kutetea haki za binadamu pamoja na mashirika ya kiraia zaidi ya 300 juma lililopita walianzisha kampeni maalumu ya kupinga hatua yoyote ile ya kumuwezesha rais Nkurunzinza kuwania urais kwa muhula wa tatu, jamabo ambalo wanasema iwapo litafanyika litakwenda kinyume na katiba ya nchi.


jeudi 12 février 2015

MVUTANO KATI YA UN NA SERIKALI YA KINSHASA KUHUSU MA JENERALI 2 WAENDELEA


Msemaji wa vikosi vya Umoja wa Mataifa nchini jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Monusco, Charles Bambara amesema Umoja wa Mataifa unafanya mapunziko katika utoaji msaada kwenye maandalizi ya mashambulizi dhidi ya kundi la waasi wa kihutu wa Rwanda waliopiga kambi mashariki mwa DRCongo.

Hivi majuzi akiwa jijini New York kiongozi mmoja wa umoja wa mataifa ambae hakupenda jina lake litajwe alisema kwamba Umoja wa Mataifa umesitisha kwa kuda utoaji msaada wake katika operesheni hiyo baada ya kutokea mvutano baina ya monusco na serikali ya Kinshasa kuhusu uteuzi wa ma jenerali wawili wa jeshi la FARDC na ambao wanatuhumiwa na Umoja wa Matifa kuhusika katika makosa ya ukiukwaji wa haki za binadamu.

umoja wa Mataifa umesema kulingana na kanuni zake haziwaruhusu kushirikiana na majenerali hao, huku kukiwa na taarifa kwamba Umoja wa Mataifa umeipa makataa serikali ya DRCongo hadi Februari 13 kuhakikisha maafisa hao wa kijeshi wamebadilishwa, la sivyo Monusco haitoshiriki katika opersheni hiyo.

Tayari serikali ya DRCongo imetupilia mbali makataa hayo kwa sababu maafisa hao jenerali Bruno Mandevu na Sikabwe Fall hawana kesi yoyote ya kujibu katika mahakama ya kijeshi.

KINACHOFANYWA NA RAIS NKURUNZIZA KWA SASA NDIO ULE MCHEZO WA NDANI?

Mkanganyiko umeendelea kushuhudiwa katika chama tawala nchini Burundi cha CNDD-FDD, chama ambacho hapo awali kilileta matumaini ya kuwau...