lundi 20 octobre 2014
mardi 7 octobre 2014
KUNDI LILILO ASI CHAMA CHA FNL LAKIRI KUHUSIKA KATIKA SHAMBULIO LA JESHI LA BURUNDI
Kundi
moja la waasi nchini Burundi, limejigamba hapo jana kuhusika katika
shambulio dhidi ya kituo kimoja cha kijeshi nchini humo karibu na
mpaka na jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, na kukiri kuwauwa
wanajeshi sita katika shambulio hilo, idadi iliokanushwa na jeshi la
taifa hilo.
Msejaji
wa jeshi la Burundi kanali Gaspard Baratuza amefahamisha kwamba
kulikuwa na makabiliano na kundi la wahuni, na kukanusha taarifa ya
kupoteza wanajeshi, badala yake kuthibitisha kuwa wamemuua muasi
mmoja katika shambulio hilo.
Kundi
hilo la waasi linasadikiwa kuwa ni miongoni mwa wafuasi wa chama cha
FNL walioasi na kuanzisha uasi. Kulingana na msemaji wa kundi hilo
Felix Jean Ntahonguriye amethibitisha kwamba walishambulia kituo cha
jeshi kilichopo katika tarafa ya Gihanga kwenye umbali wa kilometa
zaidi ya Ishirini na jiji la Bujumbura na baadae kutokomea katika
msitu wa Rukoko karibu na DRCongo.
Tangu
mwanzoni mwa mwaka huu, kundi hilo limekuwa likijigamba kuhusika na
mashambulizi kadhaa ambapo kulingana na msemaji wa kundi hilo
wataendelea kutekeleza mashambulizi dhidi ya vituo vya jeshi la
Burundi hadi kwenye uchaguzi wa mwaka 2015.
msemaji
wa jeshi la Burundi Gaspard Baratuza amepuuzia kitisho hicho na
kusema kwamba ni kundi la wahuni waliopoteza dira na haliwezi
kupambana na jeshi la serikali.
HERVE LADSOUS KUHUDHIRIA SHEREHE ZA KUAGWA KWA MIILI YA WANAJESHI WA UN JIJINI BAMAKO
Herve
Ladsous naibu katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa anaye husika na
opersheni za kulinda amani yupo nchini Mali ambako atahudhuria
sherehe za kuiaga miili ya wanajeshi tisa wa Nigeria waliouawa katika
shambulio liliotokea siku ya Ijuma juma lililopita.
Miili
ya wanajeshi hao tisa wa kulinda amani kutoka nchini Nigeria itawekwa
nje kwenye makao makuu ya vikosi vya kulinda amani jijini Bamako
ambako mawaziri Abdoulaye Diop, wa mambo ya ndani nchini Mali pamoja
na waziri wa Ulinzi Meja Kanali Bah Ndaw wanatahudhiria
Upande
wa Minsuma, mbali na Herve Ladsous atakuwepo pia Arnaud Acodjénou
naibu kiongozi wa opersheni za Umoja wa Mataifa, ambao wamekuja
kutowa heshima za mwishi kwa wanajeshi hao waliojitolea kwa ajili ya
amani barani Afrika. Herve Ladsous atatumia fursa hiyo kukutana na
rais wa Mali Ibrahima Bubakar keita.
Herve
Ladsous atajadili pia kuhusu swala la wanajeshi wa kulinda amani
kutoka nchini Tchad ambao wanatishio kurejea nyumbani baada ya
kupoteza mara kadhaa wanajeshi wake kutokana na bomu za kutegwa
ardhini zilizo tengwa na wanamgambo.
WAZIRI WA ULINZI WA ZAMANI AIKOSOA SERA YA OBAMA KUOPAMBANA NA ISLAMIC STATE
Waziri
wa zamani wa ulinzi wa serikali ya Marekani Leon Paneta na kiongozi wa zamani wa
idara ya ujasusi, ambaye kitabu chake Worthy Fights kinazinduliwa
hii leo, ameikosoa sera ya rais Obama kupambana na Ugaidi nchini Iraq
na Syria, na kuonya kwamba kwa hali ilivyo vita hivyo vinaweza kudumu
miaka 30.
wakati
vita dhidi ya kundi la IS ikipamba moto, huku wanajihadi wa hao
wakiendelea kumudu kwenye uwanja wa mapambano dhidi ya mashambulizi
ya majeshi ya muungano, waziir wa ulinzi wa zamani amejitokeza na
kuvunja ukimya kwa kutowa kauli ambayo imeighadhabisha Ikulu ya
Marekani ya White House.
lundi 6 octobre 2014
MPIGA PICHA RAIA WA MAREKANI AREJESHWA NYUMBANI BAADA YA KUAMBUKIWA NA EBOLA LIBERIA
Mpiga
picha raia wa marekani aliepata mambukizi ya virus vya Ebola nchini
Liberia amesafirishwa kuondoka jijini Monrovia, duru za mashirika ya
kibinadamu zimearifu.
Ashoka
Mukpo mwenye umri wa miaka 33 mpiga picha na ambaye aliajiriwa hivi
karibuni na kituo cha Marekani cha NBC aliwekwa katika hali ya hatari
tangu jumatano juma lililopita katika kituo cha shirika la madaktari
wasiokuwa na mipaka.
Mwenyekiti
wa kituo cha NBC Deborah Turness alifahamisha tangu siku ya Ijumaa
iliopita kwamba mpiga picha huyo atasafirishwa hadi kwenye kituo
kingine kwa ajili ya matibabu zaidi, huku wengine ambao hawaonyeshi
dalili zozote za virusi vya Ebola watarejeshwa nyumbani na kuwekwa
kqenye hali ya hatari kwa kipindi cha siku 21 kama inavtogizwa.
KUNDI LA MUJAO LAJIGAMBA KUHUSIKA KATIKA SHMBULIO LA VIKOSI VYA UN
Mpiganaji
mmoja wa kijihadi wa kundi la Mujao, moja miongoni mwa makundi yalio
kalia eneo la kaskazini mwa Mali amejigamba kuhusika na shambulio la
kujitowa muhanga dhidi ya Kikosi cha Umoja wa mataifa nchini Humo.
Shambulio
la siku ya Ijumaa dhidi ya kikosi cha Umoja wa Mataifa cha majeshi
kutoka nchini nigeria lilisababisha vifo vya watu 9.
Uongozi
wa kikosi cha Kulinda amani cha Umoja wa Mataifa Minusma, umesema
hili ni shambulio kubwa kuwahi kutokea tangu kutumwa kwa majeshi ya
Umoja wa Mataifa tangu kutumwa kwake Julay 2013.
AL SHABAB WAPOTEZA NGOME YAO MUHIMU
Askari wa Umoja wa Afrika
nchini Somalia (AMISOM) na jeshi la Somalia wamefanikiwa siku ya
Jumapili kuuteka mji wa Barawe, ngome ya mwisho ya wanamgambo wa
Al-Shebab na bandari kuu ambayo ilikuwa bado iko mikononi mwao.
Wachambuzi wa mambo wanaona
kuwa hatua hii ni pigo kwa wanamgambo wa Al-Shabab ambao walikuwa
wanatumia bandari hii kupitisha chakula, kuuza mkaa pamoja na kupokea
wapiganaji wake wa kigeni wanaoingia nchini humo.
Wachambuzi wa mambo wanaona
kuwa hatua hii ni pigo kwa wanamgambo wa Al-Shabab ambao walikuwa
wanatumia bandari hii kupitisha chakula, kuuza mkaa pamoja na kupokea
wapiganaji wake wa kigeni wanaoingia nchini humo.
Inscription à :
Articles (Atom)
KINACHOFANYWA NA RAIS NKURUNZIZA KWA SASA NDIO ULE MCHEZO WA NDANI?
Mkanganyiko umeendelea kushuhudiwa katika chama tawala nchini Burundi cha CNDD-FDD, chama ambacho hapo awali kilileta matumaini ya kuwau...

-
Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa Jean Yves Le Drian Ufaransa imetangaza kuwa itawatuma wanajeshi wake 300 kupambana na wapiganaji wa maku...
-
Penelope Cruz na Javier Bardem Ni waigizaji wakubwa katika industry ya filamu nchini Marekani, wamepigwa marufuku kurikodi katika baadh...
-
Wanajeshi wawili wa Tchad waliomo katika kikosi cha umoja wa afrika nchini Jamhuri ya afrika ya kati Misca, wamepoteza maisha jana Jumap...
-
Hii sio ya kukosa kabisa, moja miongoni mwa tamasha kubwa la mwisho wa mwaka jijini Bujumbura. Hakuna caption ndefu picha zenyewe zinajit...
-
Shuguhuli za uzinduzi wa bunge jipya nchini Libya zimeitishwa kufanyika jumatatu hii katika miji wa Tobrouk na upande wa chama cha waza...
-
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo MONUSCO unapongeza dhamira ya serikali ya DRC kuchukua pekee juk...
-
Mapigano yamezuka tena upya nchini Libya baada ya kushuhudiwa ukimya wa siku kadhaa wakati huu ujumbe wa Umoja wa Mataifa UN ukifanya z...
-
wananchi wa Beni mashariki mwa Jamhuri ya Kidemorasia ya Congo DRC, hawanaimani na kauli za viongozi wa eneo hilo baada ya kutokea kwa ...
-
Watu 22 wameripotiwa kufa mpaka muda huu baada ya ndege ya abiria inayomilikiwa na shirika la TransAsia ya nchini Taiwani kuanguka k...