vendredi 22 juillet 2016
lundi 18 juillet 2016
RAIS WA UTURUKI AAHIDI KUMALIZA KILE ALICHOKIITA VIRUSI

Hapo
jana wakati rais Erdogan akihudhuria ibada maalumu ya mazishi
kuwakumbuka raia na wanajeshi waliouawa wakati wa jaribio la
mapinduzi, amesema kuwa nchi yake inafikiria upya kurejesha adhabu ya
kifo, licha ya wasiwasi ulioneshwa na jumuiya ya Kimataifa.
Viongozi
wa dunia, akiwemo Rais wa Marekani, Barack Obama, wamealaani jaribio
la mapinduzi lililoshindikana Ijumaa ya wiki iliyopita na wanajeshi
walioasi, ambapo kwa mujibu wa Serikali watu zaidi ya 300 waliuawa.
Hata
hivyo kumekuwa na hofu ya kutekelezwa vitendo vya ukiukwaji wa haki
za binadamu kwa watuhumiwa wa jaribio hilo, baada ya kuonekana kwa
picha zikiwaonesha maofisa wa Serikali wakiwanyanyasa wanaodaiwa kuwa
ni watuhumiwa wa jaribio la mapinduzi.
Waziri
wa sheria wa Uturuki, Bekir Bozdag, amesema kuwa watu wanaokadiriwa
kufikia elfu 6 wamekamatwa katika operesheni maalumu ya kusafisha
jeshi na taasisi za Serekali ambazo anadai zimevamiwa na watu
wanaotaka kutekeleza mapinduzi, huku akionya kuwa idadi hiyo huenda
ikaongezeka.
PADRI MALU MALU KUZIKWA LEO MJINI BUTEMBO
Kabla
ya kusafirishwa hadi Butembo, mwili wa kiongozi huyo uliagwa na umati
wa watu mjini Kinshasa, wakiwemo wanasiasa na maaskofu wa kanisa
katoliki nchini DRC.
Katika
kuithamini kazi yake na juhudi nyingi za kidiplomasia alizoongoza kwa
niaba ya serikali ya nchi hiyo, Rais Joseph Kabila, amemtaja Malumalu
kama shujaa, akifananisha yale aliyoyafanya na viongozi maarufu
nchini humo kama, Emery Patrice Lumumba na marehemu Laurent Desire
Kabila.
AU WAJADILI USALAMA WA SUDANI KUSINI NA BURUNDI
Viongozi wa Umoja wa Afrika wanajdili kuhusu usalama wa Sudani Kusini na Burundi ambako mzozo wa kisiasa umeendelea kutokota katika nchi hizo, na ambapo mwenyekiti wa Umoja huo amewatolea wito viongozi wa mataifa hayo kuheshemu makubaliano na mikataba mbalimbali iliofikiwa.
wakati huo huo rais
wa Sudan Kusini, Salva Kiir na makamu wake wa kwanza wa Rais Riek
Machar, wamekubali kukutana kwa mazungumzo, ili kusaka muafaka wa
kurejesha amani nchini humo, baada ya mapigano yaliyoshuhudiwa juma
moja lililopita.
Kwa
mujibu wa mwenyekiti wa tume inayosimamia utekelezwaji wa mkataba wa
amani uliotiwa saini na viongozi hao kumaliza vita nchini humo,
Festus Mogae, amethibitisha Rais Kiir kuzungumza kwa njia ya simu na
Riek Machar na kukubaliana kukutana, wakati huu pia jumuiya ya nchi
za IGAD, ikifikiria kutuma wanajeshi elfu 14 nchini Sudan Kusini
kulinda amani.
Viongozi Wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika,
wanaotarajiwa kutamatisha kikao chao hivi leo jijini Kigali, Rwanda, wanatarajiwa kutoka na maazimio kuhusu kinachoshuhudiwa kwenye
nchi hiyo.
Hata
hivyo maswali bado ni mengi ikiwa kweli wakuu hawa wa nchi wana nia
ya dhati ya kumaliza machafuko Sudan Kusini, na kama watatoka na
maazimio mahsusi kumaliza mgogoro wa nchi hiyo.
Haji
Kaburu ni mchambuzi wa siasa za kimataifa, akiwa jijini Dar es
Salaam, Tanzania na hapa anaeleza mtazamo wake.
Inscription à :
Articles (Atom)
KINACHOFANYWA NA RAIS NKURUNZIZA KWA SASA NDIO ULE MCHEZO WA NDANI?
Mkanganyiko umeendelea kushuhudiwa katika chama tawala nchini Burundi cha CNDD-FDD, chama ambacho hapo awali kilileta matumaini ya kuwau...

-
Umoja wa Mataifa imeikosoa hatuwa ya serikali ya burundi ya kuendelea kumuweka korokoroni mkurugenzi wa kituo kimoja cha ra...
-
Polisi nchini Ufaransa, inawashikilia watu 8 wanaotuhumiwa kujihusisha na mtandao wa kusafirisha vijana kwenda nchini Syria...
-
Viongozi wa serikali ya Afrika Kusini wamesema watafanya uchunguzi kuhusu uwepo wa taarifa za ubaguzi wa rangi katika shule...
-
Baraza la Senet nchini Burundi, limeidhinisha majina ya viongozi wa idara ya upelelezi yaliowasilishwa na rais wa Burundi Pierre Nku...
-
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC imesema kuwa imekataa ombi la tume ya Umoja wa mataifa nchini humo kushirikiana na...