Pages

lundi 12 janvier 2015

HALI YA TAHARUKI YATANDA JIJINI KINSHASA

Hali ya taharuki imeendelea kutanda jijini Kinshasa karibu na biunge la taifa nchini jamhuri ya kidemokrasia ya Congo ambako polisi ya usalama imeendelea kuewatawanya wafuasi wa upinzani wanaopinga mpango wa mageuzi ya sheria ya uchaguzi ambayo ilipangwa kujadiliwa bungeni hii leo.

upinzani nchini drcongo unaona kwamba mageuzi ya sheria hiyo ya uchaguzi yatachelewesha kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa rais utaompa nafasi rais wa sasa wa nchi hiyo Joseph Kabila madarakani tangu mwaka 2001 kuendelea kusalia uongozini baada ya kutamatika kwa muhula wake wa tatu na wa mwisho mwaka 2016.

polisi wa usalama wa raia wamezuia maeneo yote yanayoelekea kwenye majengo ya bunge la taifa nchini humo Palais du peuple ambako wabunge walipanga kujadili muswada wa sheria uhusuo mabadiliko ya sheria ya uchaguzi uliowasilishwa bungeni na serikali kwa ajili ya kujadiliwa katika kikao cha bunge mchana huu.

Katika taarifa ya awali wabunge wa upinzani waliafifu kwamba watasusia cikoa hivyo vya kufanya mageuzi katiba ya nchi hiyo katika kile walichokiita kuhofia kuwa wahaini.

Mapema leo asubuhi polisi wamewasambaratisha wafuasi wa upinzani takriban 300 hivi waliokuwa wamekusanyika karibu na ofisi za bunge kwa kutumia bomu za kutowa machozi, kabla ya kukimbilia kwenye ofisi za vyama vya upinzani hususan chama cha UNC cha Vital Kamerhe ambako kumeshuhudiwa mvutano wa polisi na vijana waliochoma moto magurudumu.

Israel Mutombo Msemaji wa kiongozi wa polisi nchini humo jenerali Celsstin Kanyama amesema wamekuhamasisha idadi kubwa ya polisi nchini na kwamba hawana habari yoyote kutoka serikali inayoruhusu kufanyika kwa maandamano.



Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire

KINACHOFANYWA NA RAIS NKURUNZIZA KWA SASA NDIO ULE MCHEZO WA NDANI?

Mkanganyiko umeendelea kushuhudiwa katika chama tawala nchini Burundi cha CNDD-FDD, chama ambacho hapo awali kilileta matumaini ya kuwau...